Shingo zetu zimechongoka
asubuhi kuilekea
lakini usiku wasogea
ukichimba misingi ya nyumba,
na ukuta wa dakika nyumba
kuizunguka.
Kifo kimeadhimishwa
na ule wakati uliotandazika
mpaka
kila cha zamani kimesahaulika
isipokuwa majani makavu yalokauka
Mitini, mara kwa mara, yakitingisika
Ati n'nani aliyesikia sauti?
Kama kwamba kuna mtu huko mbinguni
wa kutulipia damu yetu iliyomwagwa
na kumwagika
***********************
Alamin Mazrui
( English Translation by
The Poetry Translation Workshop)
The Voice?
Our throats sharpentowards morning
but night approaches
digging the foundations of the house
and the wall of minutes
that surrounds the house
Death is honoured
by time stretched out
until everything past has been forgotten
other than the leaves that dried
on the tree, that tremble, now and then
Who would have heard the voice?
As if there were a person in heaven
to pay for our blood that was poured
and poured out
কোন মন্তব্য নেই:
একটি মন্তব্য পোস্ট করুন